My Web

Emmanuel

CONTACT

Monday, January 23, 2012

Wema, Kanumba wazua gumzo

Musa Mateja
PICHA mpya za pamoja walizopiga Wema Isaac Sepetu na Steven Charles Kanumba, zimezua gumzo jipya na watu wanahoji imekuwaje tena wakati ‘wanasemaga’ hawana ukaribu wowote?
Wema ‘alibipu’ na picha hizo kwenye mtandao wa BlackBerry Messenger (BBM) juzikati ili kuona kama watu watasemaje ambapo ndani ya dakika chache, alikuwa ameshambuliwa vibaya kwa maoni kibao.
Katika tukio hilo lililojiri Januari 17, mwaka huu, Wema alilazimika kuiondoa picha hiyo mara moja kwani watu walikuwa wakitaka kujua ukaribu huo ulitokana na mazingira gani.
“Umbeya mwingine bana! Watu wameshaanza kutumiana meseji kwamba baada ya kutibuana na Diamond (Naseeb Abdul), sasa Wema karudi kwa Kanumba,” ilisomeka sehemu ya maoni hayo.
Hata hivyo, Ijumaa Wikienda lilipozungumza uso kwa uso na Wema juu ya ishu hiyo, alisema kuwa alikutana na Kanumba kwenye mahojiano katika Runinga ya EATV, ndipo ‘wakafotoana’ picha hizo.
“Sipendi bifu na mwanaume niliyeachana naye, nikimwagana na mtu, haina maana kwamba hatuwezi ‘kushea’, picha tulipiga watu wengi na wala hazimaanishi nimerudiana na Kanumba,” alisema Wema aliyewahi kuwa mpenzi wa staa huyo wa muvi za Kibongo.

No comments:

Post a Comment

New