My Web

Emmanuel

CONTACT

Sunday, June 10, 2012

JANGWANI LEO

JANGWANI LEO NI MWENDO WA KUVAA UZALENDO

Hiyo ndio slogan mpya ya Chama Cha Mapinduzi ambayo inatazamiwa
kushamiri kila kona ya Jangwani Leo.

MAPEMA LEO WATU WALITOKA MAENEO MBALIMBALI
WALIFIKA JANGWANI









Hizi ni baadhi ya taswira zikionyesha vyombo mbalimbali vya usafiri
vilivyo paki kusubiria nyomi iliyoko kwenye MKutano



Kwa Lugha nyingine wanasema ni nyomi ikiwa imefurika Viwanja vya
Jangwani muda huu ambapo Mkutano unaendelea nia ni kuwapongeza
viongozi wa mashina na matawi waliochaguliwa katika uchaguzi wa CCM
ulifanyika kwa ngazi hizo mkoani Dar es Salaam.

Hao ni wanachama wa CCM ambao wako kwa wingi maeneo hayo ya
Viwanja vya Jangwani ambapo viongozi wa Chama wanatoa ufafanuzi
wa mambo mbalimbali yanayotokea nchini.Hii ni KIjiweni toka Jangwani.


Wakiwa wanawasikiliza viongozi wa CCM kwa umakini kabisa hii ni
muda huu toka Jangwani ambapo panafanyika Mkutano wa Hadhara
kwa wakazi wa Jiji La Dar es Salaam na viunga vyake

WAKINAMAMA WAKIWA WANAFANYA BIASHARA





Biashara sehemu kama hizo hazikosekani hapo ni wajasiriamali nao
wakiwa wamepnga bidhaa zao kwa ajili ya kutafuta riziki huku mkutano
ukiendelea kuhutubiwa na Mawaziri mbalimbali kutolea ufafanuzi masuala
yanayowakabili Wananchi.Hii ni Jangwani Live



Hao ni wanachama wa CHADEMA na vyma vingine wakirudisha kadi
zao kwa Nape Nnauye hiyo ni Jangwani






Hawa ni Chipukizi wakiwa wamejipanga mstari vizuri kabisa haikujulikana
mara moja kisa cha wao kujipanga namna hiyo wakati mkutano ukiendelea
Hao ni wapiga kUra wa miaka ijayo wakiandaliwa uzuri wakisimamiwa vizuri
na Mkuu wao aliesimama nyuma yao




Wakati mwingine si vibaya kupata vionjo hivi vilivyokuwa vinaendelea
kwa kijana huyu akikata uno kwa raha zake hii ni Jangwani leo hii.


Kaazii kwenu kwenu mie kwa raha zangu..wimbo ulikuwa ukichagizwa
kuwa ''CCM imekaa vizuri'' akisindikizwa kwa vingoma cheki taswira chini.


Burudani hizo zikiwa zimeshamiri hapo Jangwani.


Vijana wakipata burudani huku wengine wakipuliza vuvuzela
kuashiria furaha walizokuwa nazo katika mkutano wa hadhara
hii ni Jangwani Live.


Hizo ndizo burudani zilizokuwapo Viwanja vya Jangwani ambapo kila
aina ya mbwembwe zilikuwapo kama uonavyo vijana hao ambao walikuwa
wakizunguka huku wakicheza ngoma hiyo ya asili ambayo ni ya wenyeji wa
maeneo ya Pwani

CCM LEO WAMEZUNGUMZIA MIRADI YA MAENDELEO
VIWANJA VYA JANGWANI LEO
Waziri wa Ujenzi Mh.John Pombe Magufuli akihutubia katika
mkutano wa wachama wa CCM Jangwani leo jijini Dar es salaam
ikiwa ni moja ya mikakati ya chama kusikiliza kero za wananchi
pamoja na mfumuko wa bei na upandaji holela wa nauli na
kuelezea miradi mbalimbali inayoendelea nchini
(PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)
Waziri wa uchukuzi Mh.Harrison Mwakyembe akihutubia
katika mkutano wa wachama wa CCM jangwa leo jijini
Dar es salaam ikiwa ni mikakati ya chama kusikiliza kero
za wananchi pamoja na mfumuko ya bei na upandaji holela
wa nauli na kuelezea wananchi miradi mbalimbali inayoendelea
Katika picha kutoka kushoto ni mawaziri Prof Anna Tibaijuka,
John Magufuli na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es salaam
John Guninita.
Abdulrahman Kinana (kulia) akipeana mkono na waziri
John Magufuli kushoto.

Wanachama wa CCM wakichambua baadhi ya kadi ya
vyama pinzani zilizorudishwa na wanachama wao kama
zinavyoonekana katika picha
Waziri wa nyumba na maendeleo na makazi Profesa Anna Tibaijuka
akifafanua jambo katika mkutano huo
Viongozi wa CCM pamoja na mawaziri wakiimba katika
mkutano huo uliofanyika Jangwani jijini Dar es salaam leo

No comments:

Post a Comment

New