My Web

Emmanuel

CONTACT

Friday, July 20, 2012

PICHA MBALIMBALI ZA AJALI YA MELI





Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,
(wa pili kulia) akiwa na Viongozi Wakuu wa Serikali alipofika katika Ofisi za Shirika 
la Bandari, Malindi Unguja kupata taarifa sahihi ya ajali ya kuzama kwa Meli ya 
MV Sky Get ikitokea Dar es Salaam kuelekea Unguja.








Majeruhi wakipatiwa Mablanketi kwa ajili ya kujihifadhi baada ya kuokolewa 
katika meli ya Star Gate iliozama huko katika bahari ya Chumbe Zanzibar na
 ikiwa na abiria 250.





Majeruhi alieokolewa katika meli ya Star Gate iliozama huko katika 
bahari ya Chumbe Zanzibar na ikiwa na abiria 250. 





Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Amer Kificho pamoja na mawaziri 
mbalimbali wakiwa katika Eneo la Bandari wakishuhudia kuletwa kwa 
majeruhi mbalimbali waliookolewa katika meli ya Star Gate iliozama huko 
katika bahari ya Chumbe Zanzibar na ikiwa na abiria 250





Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idi akiwa katika Eneo 
la Bandari akishuhudia kuletwa kwa majeruhi mbalimbali waliookolewa katika 
meli ya Star Gate iliozama huko katika bahari ya Chumbe Zanzibar na ikiwa na abiria 250. 





Wananchi mbalimbali wakishuhudia tukio la kuokolewa watu waliozama 
na meli ya Star Gate huko katika hukokatika bahari ya Chumbe Zanzibar 
na ikiwa na abiria 250. 





Waziri wa Nchi Afisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk 
Mwinyihaji Makame akitoa taarifa kwa Waandishi wa Habari kuhusiana na 
kuzama kwa Meli ya Star Gate hukokatika bahari ya Chumbe Zanzibar na 
ikiwa na abiria 250. 





Askari wa Vikosi mbalimbali wakiwa katika kazi ya Uokozi kwa Abiria 
waliokuwa katika Meli ya Star Gate ambayo iliozama katika ikiwa imebeba 
abiria 250 huko katika bahari ya Chumbe Zanzibar





Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Hamad Masoud Hamad akiwa katika 
hali ya huzuni Baada ya kushiriki katika uokoaji na kuwaona Majeruhi
waliookolewa katika Meli iliozama ya Star Gate wakiteremka hapo Bandarini Zanzibar. 





Abiria aliyookoka katika Meli iliozama ya Star Gate akifarijiwa na Jamaa 
zake Baada ya kuteremka katika Meli iliowaokoa hapo Bandarini





Abiria aliyeokoka kutoka katika meli iliyozama





Abiria waliookolewa kutoka katika meli iliozama ya Star Gate katika 
bahari ya Chumbe Zanzibar 





Watalii na raia wa kigeni pia walikuwemo katika meli iliyozama hawa 
ni baadhi ya waliosalimika











Majeruhi wakiwa katika hospitali ya Mnazi Mmoja





Majeruhi wa ajali ya Meli wakiwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja 
wakipata huduma baada ya kuokolewa.














Daktari akitowa huduma ya kwanza kwa mmoja wa majeruhi wa boti iliozama





Mmoja wa Majeruhi akipata huduma ya Kwanza baada ya kuokolewa 
akiwa katika bandari ya malindi














Tagi la Shirika la Bandari likiwa katika sehemu ya tukio.





Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu Hamad Masoud akiwa katika 
boti ya Kilimanjaro akiwa sehemu ya Tukio ilipozama boti hiyo maeneo ya Chumbe.








Boti ya Fly ikiondoka katika bandari ya Zanzibar kueleke kutowa 
msada w uokoaji.





Boti iliozama ni kama hii ni ni pacha wake.





Helikopta ya Jeshi la Polisi ikiwa eneo la tukio.





Boti ya KMKM ikiwa katika zoezi la kuokowa majeruhi. 





Baadhi ya Abiria wakiwa katika moja ya chombo cha kuokolea wakielea 
baharini wakisubiri kuokolewa.





Majeruhi wakiwa katika mgongo wa boti hiyo wakisubiri kuokolewa.





Waokoaji wakiokoa moja ya maiti. wakiwa katika boti ya Kilimanjaro. 





Mwokoaji akiwa na mmoja wa maiti wa ajali hiyo.


Picture


Picha kama ilivyochukuliwa na Dkt. Mahamba akiwa kwenye ndege angani 
mara baada ya rubani kuishusha ndege usawa wa futi 2,800. 


Picture




Picture









Hizi ndizo Meli za Mv Skagit ambazo ununuzi wake uliripotiwa kwenye
 vyombo vya habari mwanzoni mwa mwaka 2011 amabo ilidaiwa kuwa
meli hizi zilinunuliwa kutoka Marekani - Washington State na moja ya
kampuni za usafiri kwa Dola laki nne kwa zote mbili ambapo zilitegemewa
kutatoa huduma za usafiri kati ya Zanzibar na Dar.

Boti hizi zilitengenezwa mwaka 1989 na kila moja ina uwezo wa kubeba
abiria 250 ziliwahi kuwekwa kwenye mtandao wa E bay kwa bei ya
Dola laki tatu kila moja lakini hazikupata wateja. Zilipotengenezwa
mwaka 1989 ziligharimu Dola milioni tano.

Picha na maelezo kwa hisani ya Zanzibar Blog.

No comments:

Post a Comment

New