My Web

Emmanuel

CONTACT

Wednesday, April 11, 2012

Utabiri wa Kanumba kuhusu kifo chake


Zakayo Magulu alie kwenye Camera.
Producer/Editor na Director msaidizi wa Marehemu Steven Kanumba ambae amefanya nae kazi kwa miaka saba mfululizo Zakayo Magulu, amesema Kanumba ni kama alijitabiria kifo chake kwenye movie yake mpya ambayo haijatoka bado.
Zakayo ameamplfy “hiyo movie inaitwa LOVE & POWER ambayo imekamilika kwa asilimia 60, ambapo stori yake inahusu Kanumba kumsaidia mwanamke figo ambapo baadae wakaingia kwenye mahusiano ya kimapenzi kama mume na mke lakini baadae Kanumba akagundua yule mwanamke ana mwanaume mwingine, sasa yule mwanamke akakasirika akamsukuma Kanumba ambae alitonesha figo na kupelekwa hospitali”

Marehemu Kanumba akiwa na Zakayo Magulu kazini.
Kwenye sentensi nyingine Magulu amesema “kilichonishangaza sasa ni kwamba kwenye sinema, Daktari aliemfanyia operesheni baada ya kupata hilo tatizo, ndio daktari huyo huyo aliekuja kumuhudumia Kanumba alipoanguka juzi nyumbani kwake, alafu kitu kingine kinachonifanya nishangae Muhimbili baada ya kufariki Kanumba wasanii wameshafika pale, msanii ambae kwenye hiyo movie alimuona Kanumba kwa mara ya mwisho akiwa amefariki dunia ndio msanii huyohuyo aitwae Kupa ambae pale Muhimbili ndio amemuona Kanumba kwa mara ya mwisho na kufunga droo ya maiti, hii ilikua inatabiri lakini sisi hatukufahamu chochote wala Kanumba hakuwahi kuongea kwamba angefariki karibuni japo kulikua kuna vitu alikua anahuzunika navyo ambavyo vilikua vikimtesa moyoni”

No comments:

Post a Comment

New